Wednesday, November 14, 2012

SAIGON ASEMA ANGEKUWA NA UWEZO ANGEWACHAPA NGUMI RICK ROSS & 2 CHAINZ…….




Asubuhi ya j5 ya leo Nov 14….mtu mzima Saigon amegonga interviews mbili ambazo kila moja amejaribu kuzungumzia mambo tofauti…interview yake ya kwanza amefanya na mtandao wa ThisIs50 ambapo ameegemea zaidi ishu yake na member wa Mobb Deep…Prodigy…interview yake ya pili amefanya ndani ya Power 105.1.
Leo nadondoka na interview yake ndani ya Power 105.1 coz nahisi alichozungumzia katika interview hiyo kina mguso wa hali ya juu…rapper huyo kutoka New York amesema angekuwa na uwezo angewachapa ngumi Rick Ross na 2 Chainz na kuwafanya mfano kwa rappers wengine wote wenye muelekeo kama wao.
Kikubwa ambacho kimepelekea Saigon kusema hivyo ni content (maudhui) ya muziki wa Rick Ross na 2 Chainz ambao yeye anauona ni hatari kwa kizazi cha sasa (teenagers)…kizazi ambacho yeye anafahamu kuwa ndo kizazi shabiki cha muziki wa HipHop na anaufananisha muziki wa rappers hao na rappers wengine wengi wanaochipuka kama uyoga hivi sasa na wenye muelekeo huo na movie za ngono.
“Iko nje ya uwezo wangu…lakini unafahamu..??ningekuwa na uwezo ningewachapa ngumi kama wasipobadili jumbe za nyimbo zao…ningependa kuwachapa ngumi kila mmoja…Rozay, 2 Chainz na yeyote anayetengeneza muziki unaoharibu watoto wetu…mi nashangaa…hawa wote wanalitegemea soko hili la hawa watoto…sote tunafahamu kuwa hata ukienda kununua movie za ngono…kuna utaratibu wake ki-umri…so inakuwaje unaimba visivyostahili kwa watoto na soko lako ni hao watoto..??sitaki kutengeneza battle na watoto wangu mwenyewe ambao wamekuwa influenced na muziki wao…nina watoto mimi ujue..??Kuna siku nilikuwa kwenye 106 & Pack…nilihuzunika sana kuona mabinti wadogo wenye miaka 13 au 14 wanafuatisha lyrics zenye maneno yanayozungumzia malaya wanavyofanya ngono…nikashtuka sana…nikawaza nani alaumiwe kwa hili..”?..amesema Saigon.
Akaongeza..”siwataji Rick Ross, 2 Chainz na wengineo pekee…bali ni mtu yeyote anayehusika na hilo…wote lao moja…kwangu mimi maendeleo ya rap ni kutafuta kinachoipandisha na kuishusha pia”.

No comments:

Post a Comment