Ile story kuhusu WORLD tour ya
Rihanna na kuipromote albam yake mpya inayotarajiwa kudrop Nov hii hivi sasa
imefika patamu kinoma.
Baada ya kudrop single ya
kwanza inayosumbua kinomanoma hivi sasa “Diamond” Rihanna alitangaza tour
aliyooiita “Diamonds World Tour” baada ya albam kuwa kitaa na alitangaza tour
hiyo kuanza mwakani 2013.
Sasa mbali na kutoa ratiba
rasmi ya tour hiyo….Rihanna pia amemtangaza rapper aliyeanzia kwenye uongozaji
wa Music Videos…ASAP ROCKY kuwa mmoja kati ya wasanii watakaoandamana nae
kunako tour hiyo.
“We Found Love” hit maker
ametangaza tour hiyo kuanzia Buffalo, New York Niagara Center March 08 na
mipango ya kupiga shows Philadelphia
Pennsylvania, Chicago Illinois na Los Angeles California.
Na baadae tour hiyo kumalizikia
Brooklyn New York Barclays Centre May 04…tiketi zimeshaanza kuuzwa na
zinapatikana kupitia LiveNation.com.
No comments:
Post a Comment